Core Values
Mfanikio ya Chama yatakuwepo endapo kutakuwepo na ushirikiano na Mshikamano wa karibu kati ya Wanachama, Bodi ya watendaji na wadau wake. ni wajibu wa kila mdau kutoa ushirikiano pale unapohitajika.
Viongozi wa Chama, Wanachama na watendaji wanapaswa kuwajibika kwa maslahi mapana ya Chama.
Mara zote Viongozi wa Chama na watendaji wake watapaswa kutoa Huduma iliyo bora kwa wanachama wake.
Shughuli za Chama Zitaendeshwa katika Hali ya Uwazi na kuzingatia misingi ya kumlinda mwanachama pamoja na kuzingatia Sheria,Kanuni na muongozo wa chama.
Bodi pamoja na watendaji watapaswa kuzingatia na kufuata viwango vya kitaalamu walivyonavyo wakati wa kuendesha shughuli za chama.
Viongozi wa chama pamoja na watendaji wanapaswa kua waaminifu wakati wa kuendesha shughuli za Chama.