Kuhamasisha Walimu wote wa Arusha wawe wamejiunga na chama ifikapo 2025
Kuhamasisha uwekaji wa Akiba, Hisa na Amana ili kuendeleza na kukuza mtaji wa Chama.
Kutoa Elimu kwa jamii nzima ili kujua umuhimu wa kujiunga na SACCOSS
Kujengea uwezo wanachama ili kutoa Mikopo yenye riba nafuu ili kuwainua Kiuchumi.
Kuhusu Sisi
Hiki ni Chama cha Kuweka na Kukopa cha Walimu wa Halmashauri ya Jiji la Arusha. Kilianzishwa tarehe 23 mwezi Julai mwaka 1997 na kupewa namba ya kuandikishwa AR.329. Kikiwa na wanachama 50, ambapo wanawake ni 38 na wanaume ni 12. Lengo kuu likiwa ni kumkomboa mwalimu wa shule za awali, shule za msingi, shule za sekondari na vyuo kuweza kujiwekea akiba na kupata mikopo yenye riba nafuu ili kujiinua kiuchumi na kijamii. Chama kimepata leseni kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika yenye namba PRI-ARS-ARS-CC-2022-854. Arusha Teachers SACCOS kina leseni ya daraja A.
Piga SimuMfanikio ya Chama yatakuwepo endapo kutakuwepo na ushirikiano na Mshikamano wa karibu kati ya Wanachama, Bodi ya watendaji na wadau wake. ni wajibu wa kila mdau kutoa ushirikiano pale unapohitajika.
Viongozi wa Chama, Wanachama na watendaji wanapaswa kuwajibika kwa maslahi mapana ya Chama.
Mara zote Viongozi wa Chama na watendaji wake watapaswa kutoa Huduma iliyo bora kwa wanachama wake.
Shughuli za Chama Zitaendeshwa katika Hali ya Uwazi na kuzingatia misingi ya kumlinda mwanachama pamoja na kuzingatia Sheria,Kanuni na muongozo wa chama.
Bodi pamoja na watendaji watapaswa kuzingatia na kufuata viwango vya kitaalamu walivyonavyo wakati wa kuendesha shughuli za chama.
Viongozi wa chama pamoja na watendaji wanapaswa kua waaminifu wakati wa kuendesha shughuli za Chama.
Maono
Hiki ndicho chombo kikuu cha maamuzi katika chama.
Ndicho chombo kinachosimamia shughuli zote za chama na inachaguliwa na mkutano mkuu kwa mujibu wa masharti ya chama.
Ndicho chombo chenye wajibu wa utendaji wa shughuli zote za chama kikiongozwa na Meneja wa chama kwa mujibu wa masharti ya chama.
Ni kamati itakayokuwa na wajumbe watatu kutoka kwenye bodi ambao watakuwa na jukumu la utoaji mikopo na ufuatiliaji wa mikopo na kutoa taarifa ya mikopo kwa bodi kwa mujibu wa masharti ya chama.
Ni jicho la wanachama katika shughuli zote za chama na inachaguliwa na wanachama kwenye mkutano mkuu kwa mujibu wa masharti ya chama.
Tunajali usalama na ustawi wako wa kifedha
Fuata hatua hizi ili kuwa mwanachama
Lazima uwe mwalimu wa Halmashauri ya Jiji la Arusha na uwe na cheki namba ili chama kiweze kupata makato yako na uwe mwaminifu, mtiifu mwenye ushirikiano na wenzake.
Maelezo kuhusu huduma za mikopo
Maelezo kuhusu mfuko wa majanga na rambirambi/majanga
Ni mchango unaolipwa mara moja unapokopa mkopo kiasi cha 1.5% ya mkopo anaokopa mwanachama, ili kuwa kinga ya majanga ya kifo. Ikitokea mwanachama aliyekopa atafariki dunia, mfuko huu wa majanga utalipa deni lililobaki.
Adhabu mbalimbali katika Chama cha Arusha Teachers SACCOS Ltd.
Motisha na mifumo inayotumika katika Chama cha Arusha Teachers SACCOS Ltd.
KILA MWANACHAMA AKIFANIKIWA KUMWINGIZA MWANACHAMA MPYA ATAPEWA MOTISHA YA SH. 10,000/-
CHAMA KINATUMIA MFUMO WA FORESIGHT NA MUVU (MFUMO WA MAENDELEO YA USHIRIKA TANZANIA NZIMA).
Wasimamizi na wadau muhimu katika Chama cha Arusha Teachers SACCOS Ltd.
Wasiliana Nasi
Kwa Mawasiliano Zaidi kwa ajili ya taarifa kuhusu chama chetu na pia kama unahitaji kujiunga na chama chetu karibu sana na usisite kutupigia simu.
+255 759 800 221Uongozi